Tuesday, April 19, 2016

BAJETI YA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KINONDONI 2016/2017 CHINI YA MEYA WA MANISPAA HIYO BONIFACE JACOB




BAJETI YA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KINONDONI 2016/2017

Halmashauri ya manispaa ya kinondoni inatarajia kutumia fedha kiasi cha Tsh billioni 248,477,433,909.00



MAPATO

Katika fedha hizo

Tsh Billioni 170,489,953,899.00 ni kutoka serikali kuu, sawa na asilimia 68.6%,

TSH Billioni 1,420,000,000.00 michango ya wananchi, sawa na asilimia 0.6%,

Tsh Billioni 64,285,690,000.00 mapato ya ndani sawa na asilimia 25.8%, huku

Tsh Billioni 12,281,790,010.00 ikitoka mfuko wa Barabara sawa na asilimia 5%,hivyo kufanya kuwa na jumla ya bajeti ya Tsh Billioni 248,477,433,909.00



MATUMIZI

Katika fedha hizo kiasi cha ;

1. Tsh Billioni 125,899,275,355.00 ni matumizi ya kawaida na mishahara ya watumishi,ambapo nisawa na asilimia 51% ya bajeti yote.

2. Tsh Billioni 122,578,158,554,00 ni fedha za kutekeleza miradi ya Maendeleo ambayo ni sawa na asilimia 49%.

3.Bajeti hii ya kiasi cha Tsh billioni 248,477,433,909,00 2016/2017 imeongezeka kutoka kwa ile ya mwaka Jana ya Tsh billioni 156,024,051,000.00 2015/2016 ambayo jumla ni sawa na ongezeko la asilimia 59%.



MCHANGANUO WA FEDHA ZA MISHAHARA NA MATUMIZI YA KAWAIDA



Tsh billioni 125,899,275,355.00

1. Tsh 19,402,653,555,00 ni matumizi ya kawaida (O.C)

2. Tsh Billioni 106,496,621,800,00 ni mishahara.



MCHANGANUO WA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO

Tsh billioni 122,578,158,554,00

1.44,8883,036,445,00 (makusanyo ya ndani)

2.76,275,122,109 (kutoka serikali kuu)

3.1,420,000,000,00 (machango wa wananchi)





MATUMIZI YA MAPATO YA NDANI YA TSH BILLIONI 64,285,690,000.00

1. Tsh 44,883,036,445.00 – Miradi ya Maendeleo sawa na asilimia 68%

2.Tsh 17,348,493,555.00 – matumizi ya kawaida sawa na asilimia 28%

3. Tsh 2,054,160,000.00 sawa na asilimia 3%



MCHANGANUO WA FEDHA KUTOKA SERIKALI KUU TSH BILLIONI 170,489,953,899.00 ikiwa ni 100%

1. Tsh 97,326,482,800.00 -mishahara ya watumishi

2. Tsh 9,170,139,000.00 matumizi ya kawaida

3. Tsh 775,743,000.00 ni fidia ya vyanzo vya Manispaa vilivyofutwa na serikali kuu.

4. Tsh 63,993,332,099.00 fedha za miradi ya Maendeleo kutoka serikali kuu

5. Tsh 12,281,790,010.00 ni ruzuku kutoka mfuko wa matengenezo ya Barbara.



BAJETI HII IMETOA VIPAUMBELE 11 2016/2017

1.UJENZI NA BARABARA

(a)Kiasi cha shillingi Billioni 5.5 kimetengwa kwa ajili ya Barabara,mitaro na madaraja.

(b)Ununuzi wa mota greda moja kwa gharama za Tsh million 600.

(c)Ununuzi wa kijiko kimoja cha kuchimba mitaro Tsh million 150



2.USAFISHAJI TAKA NGUMU NA MAJI.


(a) Kutenga kiasi cha Tsh BILLIONI 2.28 kwa ajili ya ununuzi wa MAROLI 25 (roli moja kila kata) ya kusombea takataka mitaani.

(b)Ununuzi wa gari mbili za kusaga na kubeba takataka(compactors) Tsh BILLIONI 1.2

(c) Utengaji wa fedha kwa ajili ya madeni ya makandarasi wa kubeba takataka ambao unagharimu Tsh Billioni 1.8

(d)Uchangiaji wa uanzishwaji wa dampo la kisasa Mabwepande.



3.AFYA


(a)Tiba bure kwa wazee,kuanzia Julai mosi, katika huduma hii jumla ya wazee 1000 kila kata(ambao kwa kata 34 ni wazee 34,000) watapatiwa matibabu bure katika hospitali zote za serikali katika halmashauri ya kinondoni.

(b)Tiba bure kwa wananchi kinondoni kupitia Huduma ya TIKA(Tiba kwa kadi) kwa HOSPITALI zote kubwa NNE ambazo ni Mwananyamala, Tandale,Magomeni na Sinza palestina pia na zahanati zote 16 zilizopo manispaa, kwa bima ya afya itakayochangiaa kiasi cha Tsh 40,000 kila mtu kwa mwaka mzima.

(c)Ununuzi wa Magari ya wagonjwa kwa zahanati na HOSPITALI zote

(d)Fedha za ukarabati wa HOSPITALI na zahanati zote za manispaa ya kinondoni pamoja na kuongeza sehemu za kujifungulia akina Mama (TIBA YA MAMA NA MTOTO).



4.KILIMO,MIFUGO MJINI


(a) Ujenzi wa machinjio ya kisasa ambayo itakua katika hadhi ya mfano wa kuigwa Africa mashariki eneo la Mabwepande,Tsh Bilioni 1.4



5.MAENDELEO YA JAMII


(a) Tumetenga tena fedha za mikopo ya wanawake na vijana, Tsh billioni 5.5 kama kutimiza sheria ya kurudisha asilimia 10% kwa walipa kodi.



6.UTAWALA NA UONGOZI Tsh Billioni 3.1


(a) Tumepandisha posho za wenyeviti serikali za mitaa kutoka Tsh 50,000/= (hamsini elfu) mpaka kiasi cha Tsh 100,000/= (laki moja) kila mmoja.

(b) Pia ongezeko la posho za wajumbe serikali za mitaa kutoka Tsh 5000/= (elfu tano kwa mwezi) mpaka 30,000/= (elfu thelathini).

(c)Fedha kwa ajili ya shajala (stationaries) na kodi, ofisi, Umeme kwa mitaa yote Pamoja na kuzuia tozo za huduma ya serikali za mitaa ya mhuri.



(d) KUFUTWA MICHANGO YA MWENGE KWA WANANCHI

Manispaa ya kinondoni imeamua kufuta mchango kwa wananchi wote kwa kutenga fedha za manispaa ambacho ni kiasi cha Tsh million 176.



7.MASOKO, WAMACHINGA NA BIASHARA

(a) kiasi cha Tsh Billioni 1.65

kukarabati masoko yote 23 yaliyopo halmshauri pamoja na kuweza mazingira rafiki ya wamachinga katika masoko holela ya ubungo, Mwenge, Tegeta, Kimara stop over, Manzese na Mbezi mwisho.



8.ELIMU


(a) Tsh Billioni 3 za matengenezo ya madawati 30,000 kwa sekondari na shule za msingi ambazo zitatumika kukidhi hitaji la upungufu wa madawati 28,000 lililokuwepo awali na kutatua suala la wanafunzi kukaa chini.

(b)Kutenga Tsh Billioni 1.6 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa madarasa, Vyoo vya shule za msingi na kufidia michango iliyofutwa na sera ya Elimu bure.

(c) Kutenga fedha za umaliziaji wa shule ya kidato cha tano na sita ya wasichana Mabwepande(MABWE GIRL’S)

(d) Uanzishwaji wa shule ya wavulana goba (GOBA BOYS).

(e) Manunuzi ya vifaa vya maabara kiasi cha Tsh millioni 250.



9.MIPANGO MIJI

(a) Kupanga mji wa mfano kwa kata ya mbweni na mitaa baadhi ya kata za kawe na kunduchi pamoja na utunzaji wa maeneo ya wazi, barabara na uwekaji wa taa za barabarani.

(b) Urasimishaji wa maeneo ya makazi holela (squater) kwa kata za manzese, Tandale, Mwananyamala, kijitonyama, Mabibo na Kigogo.

(c)Ufunguaji wa njia, mitaro na utwaji wa maji maeneo ya wazi yaliyomilikiwa kinyume na Sheria.



10.KUIMARISHA UKUSANYAJI WA MAPATO YA HALMASHAURI
Kutumia vyanzo vilivyopo jumla 46, kuhakikisha vinakusanywa ipasavyo kwa kubana mianya ya ukwapuaji wa fedha za umma, sambamba na uimarishaji mifumo ya ukusanyaji kwa njia ya kieletroniki.

Katika kipindi cha miezi michache tumepata mafanikio ya kupanda ukusanyaji kutoka Tsh Billioni 46, kwa mwaka 2015/2016 mpaka Tsh Billioni 64 kwa mwaka 2016/2017



11.MICHEZO NA UTAMADUNI


(a)Kusimamia na kuimarisha timu ya soka ya manispaa kutoka daraja la kwanza kwenda ligi kuu kwa msimu wa 2016/2017, imetengwa bajeti kiasi cha Tsh Millioni 200.

(b)Kukuza vipaji kupitia Sanaa zingine kwa “KURUHUSU VIJANA KUIMBA NA KUREKODI BURE”



IMETOLEWA NA

OFISI YA MSTAHIKI MEYA

BONIFACE JACOB

No comments:

Post a Comment