Wednesday, February 25, 2015

BIOMETRIC VOTER REGISTRATION SYSTEM (BVR)

Kumekuwa na sintofahamu kubwa kati ya Tume ya Uchaguzi na Vyama vya Siasa kuhusu kuwasajili watu  kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Kujifunza na kujua ukweli kuhusu uwezekano wa kuwasajili raia wa Tanzania kwenye daftari la kudumu la wapiga kura kwa ajili ya kushiriki kwenye Kura ya Maoni ya Katiba na Uchaguzi Mkuu Ujao wa Mwezi Oktoba tunaweza kujifunza kutoka kwa wenzetu Ghana ambao walifanikiwa kuwasajili Raia wao kwa kutumia mfumo huu wa Computer. 

Baadhi ya Mambo muhimu ya kuzingatiwa katika kufanikisha kusajili watu katika mfumo huu wa Computer ni :-

1. Vifaa yaani seti nzima ya Computer na vifaa vya Fingerprint.

2. Elimu ya kutumia Computer kwa Maofisa wanaoshiriki kwenye zoezi la kusajili


3. Uwepo wa Nishati ya Umeme kwenye eneo husika kwa kuzingatia kwamba vifaa hivi vinatumia Nishati ya Umeme. kwa Vijijini kunaweza kutumia Umeme wa Solar mahali ambapo hakuna nishati ya umeme wa kawaida.


4. Uwepo wa Mtandao wa Computer ili data zinazopatikana ziweze kuingizwa katika Server yaani Daftari kuu kwa wakati badala ya kutumia kutumia storage media kama flash memory kutunzia data zinazotakiwa kuingizwa katika Server.










No comments:

Post a Comment